Rukia maudhui
Luka 21:1-4

Sadaka ya Mjane

Luka 21:1-4
1
Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
2
Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
3
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.
4
Hawa watu wengine wote wametoa sadaka kutokana na wingi wa mali zao. Lakini huyu mjane ametoa kutokana na umaskini wake vyote alivyokuwa navyo, hata kile alichohitaji ili kuishi.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options