Rukia maudhui
Walawi 8:1-5

Maandalizi ya Kuwekwa Wakfu

Walawi 8:1-5
1
Bwana akamwambia Mose,
2
“Waletee Aroni na wanawe mavazi yao, mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili na kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu.
3
Kisha kusanya mkutano wote kwenye ingilio la Hema la Kukutania.”
4
Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza, na mkutano ukakusanyika kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
5
Mose akaliambia kusanyiko, “Hili ndilo Bwana ameagiza lifanyike.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options