Skip to content
Walawi 18:7-18

Walawi 18:7-18

7
“ ‘Usimvunjie heshima baba yako kwa kukutana kimwili na mama yako. Yeye ni mama yako; usiwe na mahusiano kama hayo naye.
8
“ ‘Usikutane kimwili na mke wa baba yako; hiyo itamvunjia heshima baba yako.
9
“ ‘Usikutane kimwili na dada yako, wala binti wa baba yako, au binti wa mama yako, awe amezaliwa katika nyumba hiyo au mahali pengine.
10
“ ‘Usikutane kimwili na binti wa mwanao ama binti wa binti yako; utajivunjia heshima.
11
“ ‘Usikutane kimwili na binti wa mke wa baba yako, aliyezaliwa na baba yako; huyo ni dada yako.
12
“ ‘Usikutane kimwili na dada wa baba yako; ni ndugu wa karibu wa baba yako.
13
“ ‘Usikutane kimwili na dada wa mama yako, kwa sababu ni ndugu wa mama yako wa karibu.
14
“ ‘Usimvunjie heshima ndugu wa baba yako, kwa kukutana kimwili na mke wake; yeye ni shangazi yako.
15
“ ‘Usikutane kimwili na mkwe wako, yeye ni mke wa mwanao; usiwe na mahusiano kama hayo naye.
16
“ ‘Usikutane kimwili na mke wa kaka yako; utamvunjia heshima kaka yako.
17
“ ‘Usikutane kimwili na mwanamke kisha na binti yake. Usikutane kimwili na binti wa mwanawe au binti wa binti yake; hao ni ndugu zake wa karibu. Huo ni uovu.
18
“ ‘Usimchukue dada wa mke wako kuwa mke mwenza, na kukutana naye kimwili wakati bado mke wako anaishi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options