Skip to content
Maombolezo 5:11-18

Maombolezo 5:11-18

11
Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni, na mabikira katika miji ya Yuda.
12
Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao, wazee hawapewi heshima.
13
Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia, wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni.
14
Wazee wameondoka langoni la mji, vijana wameacha kuimba nyimbo zao.
15
Furaha imeondoka mioyoni mwetu, kucheza kwetu kumegeuka maombolezo.
16
Taji imeanguka kutoka kichwani petu. Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi!
17
Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia, kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia,
18
kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa, nao mbweha wanatembea juu yake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options