Yoshua 21:34-40
34
Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa: kutoka kabila la Zabuloni, Yokneamu, Karta,
35
Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
36
kutoka kabila la Reubeni walipewa Bezeri, Yahasa,
37
Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
38
kutoka kabila la Gadi walipewa, Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu,
39
Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
40
Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili.
Settings