Skip to content
Yoshua 21:27-33

Yoshua 21:27-33

27
Koo za Walawi za Wagershoni walipewa: kutoka nusu ya kabila la Manase, Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili;
28
kutoka kabila la Isakari walipewa, Kishioni, Daberathi,
29
Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
30
kutoka kabila la Asheri walipewa, Mishali, Abdoni,
31
Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
32
Kutoka kabila la Naftali walipewa, Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano.
33
Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options