Yohana 7:2
Inaonyesha mstari 2 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Baada ya mambo haya, Yesu alikwenda sehemu mbalimbali za Galilaya. Hakutaka kwenda Uyahudi kwa sababu Wayahudi huko walitaka kumuua.
2
Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3
Hivyo ndugu zake Yesu wakamwambia, “Ondoka hapa uende Uyahudi ili wanafunzi Wako wapate kuona miujiza unayofanya.
4
Mtu anayetaka kujulikana hafanyi mambo yake kwa siri. Kama unafanya mambo haya, jionyeshe kwa ulimwengu.”
5
Hata ndugu zake mwenyewe hawakumwamini.
Settings