Skip to content
Yohana 4:40

Yohana 4:40

Inaonyesha mstari 40 pamoja na muktadha unaouzunguka.
37
Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa.
38
Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”
39
Wasamaria wengi katika mji ule wakamwamini Yesu kwa sababu ya ushuhuda wa yule mwanamke alipowaambia kwamba, “Ameniambia kila kitu nilichotenda.”
40
Hivyo wale Wasamaria walipomjia, wakamsihi akae kwao. Naye akakaa huko siku mbili.
41
Kwa sababu ya neno lake, watu wengi wakaamini.
42
Wakamwambia yule mwanamke, “Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu, bali kwa kuwa tumemsikia sisi wenyewe. Tumejua hakika kweli ya kwamba huyu ndiye Kristo, Mwokozi wa ulimwengu.”
43
Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 90 chars

Options