Rukia maudhui
Ayubu 37:21-24

Ukuu wa Mwenyezi Mungu usiochunguzika

Ayubu 37:21-24
21
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options