Ayubu 36:22-26
22
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Settings