Ayubu 36:1-15
1
Elihu akaendelea kusema:
2
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
Settings