Mungu ni mwenye haki kabisa
10
“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
11
Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
12
Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
13
Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
14
Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
15
wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
Settings