Ayubu 30:26-30
26
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
Settings