Rukia maudhui
Ayubu 30:20-24

Malalamiko dhidi ya ukatili wa Mungu

Ayubu 30:20-24
20
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options