Skip to content
Ayubu 30:20

Ayubu 30:20

Inaonyesha mstari 20 pamoja na muktadha unaouzunguka.
17
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
Settings

Reading style

Typeface

Font size 19px

Reading width 90 chars

Options