Ayubu 29:12-16
12
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
Settings