Ayubu 29:11-17
11
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
Settings