Ayubu 22:6-11
6
Umedai dhamana kwa ndugu zako bila sababu; umewavua watu nguo zao, ukawaacha uchi.
7
Hukumpa maji aliyechoka, nawe ulimnyima chakula mwenye njaa,
8
ingawa ulikuwa mtu mwenye uwezo ukimiliki nchi: mtu uliyeheshimiwa, ukiishi ndani yake.
9
Umewafukuza wajane mikono mitupu na kuzivunja nguvu za yatima.
10
Ndiyo sababu mitego imekuzunguka pande zote, hatari ya ghafula inakutia hofu,
11
ndiyo sababu ni giza sana huwezi kuona, tena ndiyo sababu mafuriko ya maji yamekufunika.
Settings