Skip to content
Ayubu 22:12-20

Ayubu 22:12-20

12
“Je, Mungu hayuko katika mbingu za juu? Juu kuliko nyota zilizo juu sana!
13
Hivyo wewe wasema, ‘Mungu anajua nini?’ Je, yeye huhukumu katika giza kama hilo?
14
Mawingu mazito ni pazia lake, hivyo hatuoni sisi atembeapo juu ya anga la dunia.
15
Je, utaifuata njia ya zamani, ambayo watu waovu waliikanyaga?
16
Waliondolewa kabla ya wakati wao, misingi yao ikachukuliwa na mafuriko.
17
Walimwambia Mungu, ‘Tuache sisi! Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?’
18
Lakini ndiye alizijaza nyumba zao na vitu vizuri, hivyo ninajitenga mbali na mashauri ya waovu.
19
“Wenye haki wanaona maangamizi yao na kufurahi, nao wasio na hatia huwadhihaki, wakisema,
20
‘Hakika adui zetu wameangamizwa, nao moto umeteketeza mali zao.’
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options