Ayubu 20:10-13
10
Watoto wake watalipa yote baba yao aliyowadhulumu maskini, nayo mikono yake itarudisha mali yote aliyonyangʼanya watu.
11
Nguvu za ujana zilizoijaza mifupa yake, zitalala naye mavumbini.
12
“Ingawa uovu ni mtamu kinywani mwake naye huuficha chini ya ulimi wake,
13
ingawa hawezi kukubali kuuachia uende, lakini huuweka kinywani mwake.
Settings