Ayubu 16:18-22
18
“Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
19
Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
20
Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
21
kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
22
“Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.
Settings