4
Unamwambia Mungu, ‘Imani yangu ni kamili nami ni safi mbele zako.’
5
Aha! Laiti kwamba Mungu angesema, kwamba angefungua midomo yake dhidi yako,
6
naye akufunulie siri za hekima, kwa kuwa hekima ya kweli ina pande mbili. Ujue hili: Mungu amesahau hata baadhi ya dhambi zako.