Skip to content
Ayubu 11:1-6

Ayubu 11:1-6

1
Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:
2
“Je, maneno haya yote yapite bila kujibiwa? Je, huyu mnenaji athibitishwe kuwa na haki?
3
Je, maneno yako ya upuzi yawafanye watu wanyamaze kimya? Je, mtu asikukemee unapofanya dhihaka?
4
Unamwambia Mungu, ‘Imani yangu ni kamili nami ni safi mbele zako.’
5
Aha! Laiti kwamba Mungu angesema, kwamba angefungua midomo yake dhidi yako,
6
naye akufunulie siri za hekima, kwa kuwa hekima ya kweli ina pande mbili. Ujue hili: Mungu amesahau hata baadhi ya dhambi zako.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options