ഉള്ളടക്കത്തിലേക്ക് പോകുക
Yeremia 4:23-26

Yeremia 4:23-26

23
Niliitazama dunia, nayo haikuwa na umbo tena ni tupu; niliziangalia mbingu, mianga ilikuwa imetoweka.
24
Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka, vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.
25
Nilitazama, wala watu hawakuwepo; kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.
26
Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa, miji yake yote ilikuwa magofu mbele za Bwana, mbele ya hasira yake kali.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options