Isaya 45:14-17
14
Hili ndilo asemalo Bwana: “Mazao ya Misri na bidhaa za Kushi, nao wale Waseba warefu, watakujia na kuwa wako, watakujia wakijikokota nyuma yako, watakujia wamefungwa minyororo. Watasujudu mbele yako wakikusihi na kusema, ‘Hakika Mungu yu pamoja nawe, wala hakuna mwingine; hakuna Mungu mwingine.’ ”
15
Hakika wewe u Mungu unayejificha, Ee Mungu na Mwokozi wa Israeli.
16
Wote watengenezao sanamu wataaibika na kutahayarika; wataenda kutahayarika pamoja.
17
Lakini Israeli ataokolewa na Bwana kwa wokovu wa milele; kamwe hutaaibika wala kutatahayarika, milele yote.
Settings