Isaya 32:16-20
16
Haki itakaa katika jangwa, na uadilifu utakaa katika shamba lenye rutuba.
17
Matunda ya haki yatakuwa amani, matokeo ya haki yatakuwa utulivu na matumaini milele.
18
Watu wangu wataishi katika makao ya mahali pa amani, katika nyumba zilizo salama, katika mahali pa kupumzika pasipo na usumbufu.
19
Hata kama mvua ya mawe iangushe msitu na mji ubomolewe kabisa,
20
tazama jinsi utakavyobarikiwa, ukipanda mbegu yako katika kila kijito, na kuwaacha ngʼombe wako na punda wajilishe kwa uhuru.
Settings