Rukia maudhui
Isaya 24:17-20

Hofu Isiyokwepeka na Kuanguka kwa Ulimwengu

Isaya 24:17-20
17
Hofu, shimo na mtego vinakungojea, ewe mtu ukaaye duniani.
18
Kila akimbiaye asikiapo sauti ya hofu atatumbukia shimoni, naye yeyote apandaye kutoka shimoni, atanaswa kwenye mtego. Malango ya gharika ya mbinguni yamefunguliwa, misingi ya dunia inatikisika.
19
Dunia imepasuka, dunia imechanika, dunia imetikiswa kabisa.
20
Dunia inapepesuka kama mlevi, inayumbayumba kama kibanda kwenye upepo; imelemewa sana na mzigo wa hatia ya uasi wake na ikianguka kamwe haitainuka tena.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options