Hosea 8:1-4
1
“Wekeni tarumbeta midomoni mwenu! Tai yuko juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja Agano langu, wameasi dhidi ya sheria yangu.
2
Israeli ananililia, ‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’
3
Lakini Israeli amekataa lile lililo jema, adui atamfuatia.
4
Wanaweka wafalme bila idhini yangu, wamechagua wakuu bila kibali changu. Kwa fedha zao na dhahabu wamejitengenezea sanamu kwa ajili ya maangamizi yao wenyewe.
Settings