1
“Wekeni tarumbeta midomoni mwenu! Tai yuko juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja Agano langu, wameasi dhidi ya sheria yangu.
2
Israeli ananililia, ‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’
3
Lakini Israeli amekataa lile lililo jema, adui atamfuatia.