Rukia maudhui
Waebrania 10:1-4

Sheria ni Kivuli cha Mambo Mema

Waebrania 10:1-4
1
Sheria ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kwa njia ya dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu.
2
Kama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi.
3
Lakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka,
4
kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options