Mwanzo 28:6-9
6
Sasa Esau akajua kuwa Isaki amembariki Yakobo na kumtuma kwenda Padan-Aramu ili achukue mke huko na kwamba alipombariki alimwamuru akisema, “Usioe mke katika binti za Wakanaani,”
7
tena kwamba Yakobo amewatii baba yake na mama yake naye amekwenda Padan-Aramu.
8
Esau akatambua jinsi ambavyo baba yake Isaki anavyowachukia binti za Wakanaani.
9
Ndipo Esau akaenda kwa Ishmaeli, akamwoa Mahalati, ndugu wa Nebayothi na binti wa Ishmaeli mwana wa Abrahamu, kuongezea wale wake wengine aliokuwa nao.
Settings