Skip to content
Mwanzo 27:1-4

Mwanzo 27:1-4

1
Isaki alipokuwa mzee na macho yake yalipokuwa yamekosa nguvu asiweze kuona tena, akamwita Esau mwanawe mkubwa, akamwambia, “Mwanangu.” Akajibu, “Mimi hapa.”
2
Isaki akasema, “Mimi sasa ni mzee na sijui siku ya kifo changu.
3
Sasa basi, chukua silaha zako, podo na upinde, uende nyikani, ukawinde nyama pori kwa ajili yangu.
4
Uniandalie aina ya chakula kitamu nikipendacho uniletee nile, ili niweze kukubariki kabla sijafa.”
Settings

Reading style

Typeface

Font size 19px

Reading width 90 chars

Options