Skip to content
Mwanzo 21:17-20

Mwanzo 21:17-20

17
Mungu akamsikia kijana akilia, malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni na kumwambia, “Kuna nini Hagari? Usiogope, Mungu amesikia kijana analia akiwa amelala pale.
18
Mwinue kijana na umshike mkono, kwa maana nitamfanya kuwa taifa kubwa.”
19
Ndipo Mungu akamfumbua Hagari macho yake naye akaona kisima cha maji. Hivyo akaenda akajaza kiriba maji na kumpa kijana anywe.
20
Mungu akawa pamoja na huyu kijana alipokuwa akiendelea kukua. Aliishi jangwani na akawa mpiga upinde.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options