Rukia maudhui
Mwanzo 1:14-19

Siku ya nne: Mianga ya mbinguni

Mwanzo 1:14-19
14
Mungu akasema, “Iwepo mianga kwenye nafasi ya anga ili itenganishe usiku na mchana, nayo iwe alama ya kutambulisha majira mbalimbali, siku na miaka,
15
nayo iwe mianga kwenye nafasi ya anga ya kutia nuru juu ya dunia.” Ikawa hivyo.
16
Mungu akafanya mianga miwili mikubwa: mwanga mkubwa utawale mchana, na mwanga mdogo utawale usiku. Pia Mungu akafanya nyota.
17
Mungu akaiweka katika nafasi ya anga iangaze dunia,
18
itawale usiku na mchana, na ikatenganishe nuru na giza. Mungu akaona kuwa hili ni jema.
19
Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya nne.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options