Skip to content
Wagalatia 5:2

Wagalatia 5:2

Inaonyesha mstari 2 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Kristo alitupa uhuru, akataka tubaki huru. Hivyo simameni imara wala msikubali tena kulemewa na kongwa la utumwa.
2
Sikilizeni! Mimi, Paulo, nawaambieni kwamba kama mkikubali kutahiriwa, basi Kristo hatawafaidia chochote.
3
Namshuhudia tena kila mtu anayekubali kutahiriwa kwamba inampasa kushika sheria yote.
4
Ninyi mnaotafuta kuhesabiwa haki kwa njia ya sheria mmetengwa na Kristo, mko mbali na neema ya Mungu.
5
Kwa maana, kwa njia ya Roho kwa imani, tunangojea kwa shauku tumaini la haki.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options