Skip to content
Wagalatia 5:18-26

Wagalatia 5:18-26

18
Lakini kama mkiongozwa na Roho, hamko chini ya sheria.
19
Basi matendo ya mwili ni dhahiri nayo ni haya: Uasherati, uchafu, ufisadi,
20
kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
21
husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine yanayofanana na hayo. Nawaonya, kama nilivyokwisha kuwaonya kabla, kwamba watu watendao mambo kama hayo, hawataurithi Ufalme wa Mungu.
22
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23
upole na kiasi. Katika mambo kama haya hakuna sheria.
24
Wote walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili na shauku zake pamoja na tamaa zake.
25
Kwa kuwa tunaishi kwa Roho, basi, tuenende kwa Roho.
26
Tusijisifu bure, tukichokozana na kuoneana wivu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options