Skip to content
Wagalatia 5:13

Wagalatia 5:13

Inaonyesha mstari 13 pamoja na muktadha unaouzunguka.
10
Nina hakika katika Bwana kwamba hamtakuwa na msimamo mwingine. Mtu anayewachanganya anastahili adhabu, hata awe nani.
11
Lakini ndugu zangu, kama mimi bado ninahubiri kuhusu kutahiriwa, kwa nini bado ninateswa? Katika hiyo hali basi, kwazo la msalaba limeondolewa.
12
Laiti hao wanaowavuruga wangejihasi wao wenyewe!
13
Ndugu zangu, ninyi mliitwa ili mwe huru, hivyo msitumie uhuru wenu kama fursa ya kufuata tamaa za mwili, bali tumikianeni ninyi kwa ninyi kwa upendo.
14
Kwa maana sheria yote hukamilika katika amri moja: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.”
15
Kama mkiumana na kutafunana, angalieni, msije mkaangamizana.
16
Kwa hiyo nasema, enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options