Rukia maudhui
Kutoka 25:11-17

Kutoka 25:11-17

11
Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka.
12
Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
13
Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
14
Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
15
Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
16
Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.
17
“Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options