Skip to content
Kutoka 2:1-4

Kutoka 2:1-4

1
Basi mtu mmoja wa nyumba ya Lawi akaoa mwanamke Mlawi,
2
naye mwanamke huyo akapata mimba, akazaa mtoto wa kiume. Alipoona mtoto huyo ni mzuri, akamficha kwa miezi mitatu.
3
Lakini alipoona hawezi kumficha zaidi, akamtengenezea kisafina cha mafunjo, akakipaka lami. Kisha akamweka huyo mtoto ndani yake, akakificha katikati ya matete kando ya ukingo wa Mto Naili.
4
Dada ya huyo mtoto akasimama mbali ili kuona kitakachompata mtoto.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options