Skip to content
Kumbukumbu 31:3

Kumbukumbu 31:3

Inaonyesha mstari 3 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Kisha Mose akaenda akasema maneno haya kwa Waisraeli wote:
2
“Sasa nina miaka mia moja na ishirini nami siwezi tena kuwaongoza. Bwana ameniambia, ‘Hutavuka Yordani.’
3
Bwana Mungu wenu, yeye mwenyewe atavuka mbele yenu. Ataangamiza mataifa haya mbele yenu, nanyi mtaimiliki nchi yao. Pia Yoshua atavuka mbele yenu, kama Bwana alivyosema.
4
Naye Bwana atawafanyia watu hao kile alichowafanyia Sihoni na Ogu, wafalme wa Waamori, ambao aliwaangamiza pamoja na nchi yao.
5
Bwana atawakabidhi kwenu, nanyi lazima mwatendee yale yote niliyowaamuru.
6
Kuweni imara na moyo wa ushujaa. Msiogope wala msifadhaike kwa sababu yao, kwa kuwa Bwana Mungu wenu anakwenda pamoja nanyi; kamwe hatawaacha wala hatawatupa ninyi.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 90 chars

Options