Danieli 2:20-22
20
na akasema: “Lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; hekima na uweza ni vyake.
21
Yeye hubadili nyakati na majira; huwaweka wafalme na kuwaondoa. Huwapa hekima wenye hekima, na maarifa wenye ufahamu.
22
Hufunua siri na mambo yaliyofichika; anajua yale yaliyo gizani, nayo nuru hukaa kwake.