Matendo 9:33-35
33
Huko alimkuta mtu mmoja aitwaye Ainea, ambaye alikuwa amepooza na kwa muda wa miaka minane alikuwa hajaondoka kitandani.
34
Petro akamwambia, “Ainea, Yesu Kristo anakuponya, inuka utandike kitanda chako.” Mara Ainea akainuka.
35
Watu wote wa Lida na Sharoni walipomwona Ainea akitembea wakamgeukia Bwana.
Settings