Matendo 19:4-7
4
Paulo akasema, “Ubatizo wa Yohana ulikuwa wa toba, aliwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja baada yake, yaani, Yesu.”
5
Waliposikia haya, wakabatizwa katika jina la Bwana Yesu.
6
Paulo alipoweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akawashukia, nao wakanena kwa lugha mpya na kutabiri.
7
Walikuwa kama wanaume kumi na wawili.
Settings