Matendo 10:11-16
11
Akaona mbingu zimefunguka na kitu kama nguo kubwa kikishushwa duniani kwa ncha zake nne.
12
Ndani yake walikuwepo aina zote za wanyama wenye miguu minne, nao watambaao nchini, na ndege wa angani.
13
Ndipo sauti ikamwambia “Petro, ondoka, uchinje na ule.”
14
Petro akajibu, “La hasha Bwana! Sijawahi kamwe kula kitu chochote kilicho najisi.”
15
Ile sauti ikasema naye mara ya pili, “Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.”
16
Jambo hili lilitokea mara tatu na ghafula ile nguo ikarudishwa mbinguni.
Settings