Skip to content
2 Samweli 23:1

2 Samweli 23:1

Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
2
“Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
3
Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
4
yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options