Skip to content
2 Samweli 22:47-51

2 Samweli 22:47-51

47
“Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
48
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
49
aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
50
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
51
Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options