Skip to content
2 Samweli 22:31-46

2 Samweli 22:31-46

31
“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
32
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
33
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
34
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
35
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
36
Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
37
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
38
“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
39
Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
40
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
41
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
42
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
43
Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
44
“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
45
nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
46
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options