Skip to content
2 Wakorintho 3:12-15

2 Wakorintho 3:12-15

12
Kwa hiyo, kwa kuwa tunalo tumaini hili, tuna ujasiri sana.
13
Sisi si kama Mose, ambaye ilimpasa kuweka utaji ili kufunika uso wake ili Waisraeli wasiuone ule mngʼao uliokuwa juu yake hadi ulipofifia na hatimaye kutoweka.
14
Lakini akili zao zilipumbazwa, kwa maana mpaka leo utaji ule ule hufunika wakati Agano la Kale linasomwa. Huo utaji haujaondolewa, kwa maana ni katika Kristo peke yake unaondolewa.
15
Hata leo Sheria ya Mose inaposomwa, utaji hufunika mioyo yao.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options