Skip to content
1 Wathesalonike 5:12-22

1 Wathesalonike 5:12-22

12
Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya.
13
Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi.
14
Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote.
15
Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
16
Furahini siku zote;
17
ombeni bila kukoma;
18
shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.
19
Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu;
20
msiyadharau maneno ya unabii.
21
Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema.
22
Jiepusheni na uovu wa kila namna.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options