1 Wathesalonike 5:1-3
1
Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia,
2
kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku.
3
Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.
Settings